Tuesday 4 August 2015

Fahamu Umuhimu wa Lishe na Mfumo wa Maisha Katika Kutibu Ugumba kwa Wanawake


Image result for pregnant woman photos

Je, Unafahamu kwamba unaweza kuondokana na tatizo la ugumba kwa kupitia ulaji wa vyakula na kubadiri mfumo wa maisha yako bila hata kutumia tiba yoyote? soma mada hii...

Tatizo la kukosa kuzaa au ugumba (Infertility) ni hali inayowapata wanandoa (mwanaume na mwanamke) kufuatia mwanamke kutoshika ujauzito kwa muda wa mwaka mmoja licha ya kufanya tendo la ndoa na mume wake mara kwa mara ndani ya kipindi hicho. Tatizo la ugumba (Infertility) huathiri takriban ndoa moja kati ya ndoa sita kwa wastani. Mwanaume ana asilimia 40 ya chanzo cha tatizo na mwanamke pia ana asilimia 40. Asilimia 20 zinazobaki zinatokana na vyanzo vingine mbali na mwamnamke au mwanaume. Kwa wanawake tatizo la kukosa kuzaa hutokana na hitilafu kwenye mayai au mifuko ya mayai (Ovarian disorders) na kwa upande wa wanaume tatizo hutokana na matizo yatokanayo na uzalishaji wa shahawa.


Takriban theluthi moja (1/3) ya tatizo la ugumba kwa mwanamke (female infertility) hutokana na yai kutokupevushwa ambayo kitalaamu huitwa ‘Onovulation’. Ili yai lipevushwe na kuwa tayari kurutubishwa na shahawa za mwanaume homoni za mwanamke zinapaswa kuwa katika uwiano unafaa (balance of hormones). Tatizo la kutokuwiana kwa homoni (hormonal imbalance) hupelekea mwanamke kushindwa kutunga mimba.

Tezi ndogo mbili aambazo ziko katika ubongo ziitwazo ‘hypothalamus’ na ‘pituitary gland’ husimamia uzalishaji na utendaji kazi wa homoni. Hypothalamus huzalisha homoni ya masuala ya uzazi iitwayo ‘gonadotropin-releasing hormone (GnRH)’ ambayo huchochea tezi ya pituitary kupeleka meseji kwa mayai ya mwanamke (ovaries).   Ovaries hujibu meseji kwa kuivisha yai na kuachilia yai hilo kwenye mirija ya uzazi (fallopian tubes) kwa ajili ya kurutubishwa. Yapo mambo kadhaa ambayo yanaweza kuingilia utendaji kazi wa hypothalamus hivyo kukwaza tezi hiyo kushindwa kuwasilisha meseji sahihi kwa tezi ya pituitary. Mambo hayo ni pamoja na hali ya mawazo kutokana na kukwazwa na mwenzi (emotional stress), mazoezi makali ya viungo, kujibana lishe (dieting), lishe duni, mwili kuwa na mafuta kidogo (low body fat), anorexia, matumizi ya madawa (medications) na sumu za kimazingira (environmental toxins).

Tezi ya pituitary huchangia utungaji mimba kwa kuzalisha homoni mbili ziitwazo ‘follicle-stimulating hormone (FSH) na ‘luteinizing hormone (LH)’. Homoni hizi huchochea follicles katika ovaries kupevusha na kuachilia mayai yaliyokomaa kwa ajili ya kurutubishwa. Pia hutoa amri kwa ovaries kuzalisha homoni ziitwazo ‘Estrogen’ (homoni ya kike) na ‘Progesterone’ (homoni ya kiume). Hitilafu au kushindwa kufanya kazi sawasawa kwa tezi ya Pituitary huweza kusababisha tezi hiyo ama kuzalisha kwa kiwango cha juu (over-produce) au katika kiwango cha chini (under-produce) FSH na LH, hivyo upevushaji wa mayai kushindwa kufanyika.


Tezi nyingine iitwayo thyroid endapo itatokea kuwa inafanya kazi sana kuliko ipasavyo (hyperthyroid) au inafanya kazi chini ya kiwango chake cha ufanisi (hypothyroid) husababisha mwili kushindwa kutumia ipasavyo homoni hivyo kuleta tatizo la mwanamke kushindwa kutunga mimba. Kila mwanamke ana kiasi kidogo cha homoni za kiume ziitwayo androgens. Homoni hizi ziko ndani ya damu na kuzunguka katika mzunguko wa kawaida wa damu. Homoni hizi huzalishwa na tezi iitwayo Adrenal. Endapo tezi za adrenal zitashindwa kufanya kazi sawasawa hali hiyo itasababisha upevushaji wa yai kuathiriwa. Uzalishaji mkubwa kuliko kawaida wa tezi hiyo katika mwili ni dalili kwamba mwanamke husika ana tatizo liitwalo ‘Polycystic ovary syndrome’, tatizo ambalo hupelekea mwanamke kushindwa kushika ujauzito.

Yapo matatizo mbalimbali ya ovari (Ovarian disorder) ikiwa ni pamoja na makovu (cysts), tumor, maambukizi, na maradhi yanayoathiri uzazi. Baadhi ya wanawake hupatwa na tatizo la kushika ujauzito kutokana na mifuko yao ya uzazi (ovari) kushindwa kufanya kazi kutokana na upasuaji (surgery), majeraha waliyowahi kupata (injury), mionzi (radiation) au matatizo ya kibaolojia (chromosomal problems), kuishiwa mayai mapema na kupelekea kuingia katika hali ya kukoma kuzaa (menopause) kabla ya wakati. Katika hali ya nadra sana baadhi ya wanawake huzaliwa wakiwa hawana mifuko ya uzazi (ovaries) au kutokuwa na mayai ya kutosha. Mimba ya mtoto wa jinsia ya kike ikifikia miezi mitano mtoto huyo wa kike huwa na mayai ya uzazi katika kifuko chake cha mayai (fetal ovaries) zaidi ya milioni 7. Mtoto huyo akizaliwa na kufikia umri wa kubalehe mayai hayo huwa mengine yameungana na kufanya idadi ya mayai kupungua hadi laki 3.

Kadhalika mapungufu ya mji wa mimba (uterus) pia huweza kusababisha mwanamke kushindwa kushika mimba. Katika hali ya kawaida ya mchakato wa uzazi homoni za progesterone na luteinizing hormone (LH) huchochea kuta za mji wa mimba kuongezeka unene (uterine lining thickening) ili kuwezesha yai lililorutubishwa kujishikiza kwenye kuta. Endapo mji wa mimba (uterus) hauna maelewano na homoni hizo hali hiyo hupelekea yai kushindwa kujishikiza na hatima yake ni mimba kutoka (spontaneous abortion or miscarriage). Wanawake wengine wana miji ya mimba isiyokuwa na maumbile kamilifu (structurally abnormal) na wengine hawana kabisa miji ya mimba, hali hizi zote husababisha kutokushika ujauzito.

Magonjwa ya ngono (Sexually transmitted diseases – STDs) kama vile gonorrhea, Chlamydia na Pelvic inflammatory disease (PID) huathiri hali ya wanawake kushika ujauzito. Maambukizi haya huweza kudumu katika miili ya wanawake kwa kipindi kirefu bila wahusika kujitambua hali ambayo huweza kusababisha makovu kwenye mji wa mimba (scar), kuziba kwa milija ya uzazi (block fallopian tubes) na kusabisha ‘formation of pelvic adhesions’. Kadhalika maambukizi ya mara kwa mara ya fangasi (yeast infections) kitalaam ‘Vaginitis’ huweza kuharibu milija ya uzazi hivyo mbegu za kiume kushindwa kupenya ili zikarutubishe yai. Matatizo mengine yanayoweza kupelekea milija kuziba ni pamoja na upasuaji wa tumbo au nyonga (Abnominal or pelvic surgery), Appendicitis, Endometriosis, Ectopic pregnancies au matumizi ya vifaa vya uzazi wa mpango (IUD contraceptive device). Matumizi ya vidonge vya majira husababisha ugumba wa muda (temporary infertility) kwa kipindi cha hadi miezi sita.

Wanawake wengi hawaelewi kwamba lishe, viini lishe (nutrition) na mfumo wa maisha kuchangia tatizo la ugumba. Mazoezi makali (Excessive exercises), ‘low –calorie diet’, ulaji usifaa (eating disorder), fetma (Obesity), matumizi ya aina fulani ya madawa, mawazo yaliyopitiliza kutokana na kuudhiwa (elevated stress levels) na matumizi ya mafuta ya kulainisha uke (vaginal lubricants) pia huathiri mfumo wa uzazi wa mwanamke. Cases nyingi za ugumba husababishwa na wanandoa kushindwa kufanya timing ya siku za kujamiiana ili mwanamke kupata ujauzito. Katika mwaka mzima (siku 365) mwanamke ana siku 26 tu za kutungishwa ujauzito. Siku zingine zinaobaki yaani 339 ni siku potevu (waste days). 

Tiba ya Lishe kwa Wanawake Katika Kutibu Ugumba.
Kuwa na Uzito Unaostahili Ili kupata Ujauzito
Uzito wa mwili unaathiri uwezo wa mwanamke kupata ujauzito. Kama una uzito mkubwa kuliko upasavyo kuwa (Obese) seli za mafuta katika mwili huzalisha homoni nyingi ya estrogen ambayo hukwaza uwezo wa kutunga mimba. Kiwango cha juu cha estrogen hupeleka ujumbe kwenye ubongo kusitisha kuchochea development of follicles. Hali hiyo hufanya kutokutokea kwa upevushaji wa mayai. Hali hii huwapata zaidi wanawake wenye tatizo la ‘Polycystic ovary syndrome (PCOS)’.  Tafiti zimeonyesha kwamba wanawake wenye uzito mkubwa (Obese) wakipunguza uzito wao kufikia kiwango kinachotakiwa hali ya upevushaji wa yai hurudi tena na mwanamke kushika ujauzito.

Mwanamke kuwa na uzito mdogo kuliko kawaida mafuta mwilini ambayo ni muhimu kwa upevushaji wa mayai nayo huwa katika kiasi kidogo na homoni zinazohusika na uzazi huathirika kiutendaji kazi na matokeo yake ni mwanamke kuwa mgumba.

Matumizi ya Caffeine na Alcohol na Uvutaji Sigara
Tafiti zimedhibitisha kwamba utumiaji wa caffeine zaidi ya 300 milligrams kila siku (sawa na kinywaji cha kahawa vikombe 2) husababisha uchelewaji wa mwanamke kutunga ujauzito. Utafiti uliofanywa katika Chuo Kikuu cha Johns Hopkins kuhusu wanawake waliotumia caffeine zaidi ya 300 milligrams dhidi ya wale waliotumia caffeine chini ya kiwango hicho. Matokeo yalibainisha kwamba utungaji mimba kwa mwezi kwa wanawake waliotumia caffeine zaidi ya 300milligrams kwa siku ulipungua kwa asilimia 25.
Utafiti uliofanywa katika Chuo cha Harvard School of Public Health walifanya utafiti kwa wanawake zaidi ya 4000 waliotumia alcohol na kubaini kwamba wanawake waliotumia kilevi kiasi cha chupa mbili kwa siku waliathiri uwezo wao wa kupata ujauzito kuliko wale ambao hawakuwa wakitumia kabisa pombe. Ndio kusema kwamba kadiri mwanamke anavyotumia kilevi zaidi ndivyo tatizo linazidi kuwa kubwa.
Tafiti zimethibitisha kwamba wanawake wanaovuta sigara huku wakijaribu kupata ujauzito huchelewa kupata ujauzito. Kadhalika uvutaji sigara kwa wanawake huathiri afya na utendaji kazi wa ovari na kufanya uharibifu kwenye mayai ya uzazi na kuathiri homoni ya kike ya estrogen. Hivyo wanawake wanaotaka kutunga ujauzito na huku ni watumiaji wa sigara wanashauriwa kuacha uvutaji wa sigara.

Vitamin B12.
Upungufu wa Vitamin B12 kwa mwanamke husababisha tatizo la kupata ujauzito. Wanawake walio katika umri wa kutunga mimba wanapaswa kutumia 2.4 micrograms za vitamin B12 kila siku. Aina hiyo ya vitamin hupatikana kwenye vyakula vitokanavyo na wanyama (animal foods) au kwa kutumia vidonge vya vitamin mbalimbali (Vitamin B complex).
Vyakula vilivyo na vitamin B12 ni pamoja na nyama, kuku, samaki, bidhaa za maziwa, mayai, soya na maziwa ya mchele (rice milk).

Tiba Mbadala (Herbal Remedies)

Chasteberry ni mmea tiba muhimu kwa wanawake kwa masuala mbalimbali yahusuyo uzazi. Mmea huo hutibu pamoja na matatizo mengine, kukosa mzunguko wa siku za hedhi ( Absence of menstrual periods – Amenorrhea), kutokuwiana kwa homoni (hormones imbalance), menstrual irregularities, na lower excessive level of prolactin. Nchini Ujerumani mmea huo uliweza kutibu wanawake 10 kati 15 waliokuwa na tatizo la kutokupata siku za hedhi. Mwanamke mwenye matatizo ya hayo hapo juu anashauriwa kutumia 175-225 milligrams kwa siku. Tiba hii haileti matokeo ya mara moja kwa haraka bali huchukua takriban miezi 5-7 kuona matokeo ya tiba. Aidha kwa mwanamke ambaye amekosa siku zake kwa kipindi cha zaidi ya miaka miwili itamchukua miezi 18 kuona matokeo chanya ya tiba hiyo. Mara tu baada ya kupata ujauzito mwanamke anapaswa kuacha kutumia tiba hii.

No comments:

Post a Comment