Tuesday 4 August 2015

Mambo Muhimu Ya Kufanya Kuondokana na Tatizo la Fetma...Part 3

Hii ni sehemu ya mwisho ya mada kuhusu namna ya kuondokana na tatizo la Fetma (obesity). ukifanya mambo niliyoyaeleza kwenye part 1 hadi part 3 ambayo ndio hii unayoisoma hakika utaondokana na tatizo la unene hata kama tatizo hilo limekuwa sugu licha ya kufanya jitihada mbalimbali za kuliondoa. Sasa endelea....


Chakula au Juisi ya Kukata Tatizo la Hamu/Uchu wa Vyakula
          Ipo njia moja tu ya kuondokana kabisa na tatizo la hamu au uchu wa vyakula ambayo ni kuondoa taka za asidi mwilini kwa kuufanya mwili uwe na alkali yaani ‘to alkalize your body to eliminate food cravings’. Unapaswa ufuate hatua mbili ili kuondokana kabisa na tatizo la uchu wa vyakula, moja ni kuchagua aina ya vyakula kulingana na uwezo wa mwili wako kuyeyusha vyakula hivyo (customize your diet to your own digestive metabolism). Hatua ya pili ni jenga tabia ya ku-alkalize mwili wako mara kwa mara kwa kutumia mlo wa viazi vyeupe (white potatoes). Ipo aina tatu za milo ya viazi ambayo nitaileza na jinsi ya kuiandaa. Kila aina ya mlo wa viazi vyeupe una tofautiana kidogo na aina nyingine kwa upande wa manufaa ya kiafya na pia hutofautiana kwa muda/kipindi mpaka manufaa yake kuonekana.
  1. Viazi vilivyoiva Nusu (Semi-Raw Potatoes)
Manufaa ya aina hii ya mlo wa viazi ni ya muda mrefu. Unahitaji kutumia mlo huu kila siku kwa kipindi cha miezi 2 hadi mitano ili kufikia utatuzi wa tatizo la uchu wa chakula au kupunguza tatizo la kupatwa njaa mara kwa mara. Lakini pia mlo huu hutibu tatizo la gesi au kiungulia ndani ya kipindi cha wiki chache tu. Kwa watu wenye tatizo la kupatwa na asidi (acid reflux) huu ni mlo mzuri kwao kwani huyeyushwa vizuri mwilini.
Namna ya kuandaa: kata viazi (potatoes) katika vipande vidogo vidogo, ikiwezekana usivimenye maganda yake. Weka kwenye chombo cha kupikia. Weka maji lakini yasifunike viazi. Pika kwa kutumia moto usio mkali taratibu mpaka vianze kuwa laini lakini visiive mpaka ndani. Kisha ipua. Kula viazi na kunywa maji uliyopikia. Usiyamwage hayo maji.

  1. Grated Potatoes
Hapa ni kwamba viazi vinakuwa kama vinasagwa au katwakatwa katika vipande vidogo vidogo kama ambavyo karoti husagwa. Vipande vipande hivyo vya viazi vina mucilage nyingi na husaidia kukata hamu ya vyakula ndani ya siku tatu au nne.
Namna ya kuandaa: Menya viazi kuondoa maganda yake. Hii hufanya viazi kuachilia mucilage nyingi zaidi. Kisha baada ya kuvimenya visage kwa kutumia kifaa cha kusagia (grate the potatoes). Kusaga viazi hufungua fiber za viazi kiasi kwamba joto wakati wa kuvipika hufanya mucilage kuachiliwa zaidi. Weka vipande vya viazi kwenye ‘an 8-inch frying pan’. Weka maji lakini usifunike viazi hivyo. Funika. Pika kwa joto la juu kidogo na pale maji yakianza kuchemka subiri dakika 2-3 kisha punguza joto (medium to low). Endelea kupika kwa dakika zingine 5-10. Mara nyingine itakulazimu kuwa unaongeza maji kidogo kidogo hadi viazi viive. Kwa aina hii ya mlo, viazi huiva kabisa. Lengo sio kutunza (preserve) vimeng’enywa (enzymes) na vitamin bali lengo ni kupata mucilage nyingi zaidi kadri iwezekanavyo kutoka kwenye viazi.
Namna ingine ya kuandaa mlo huu: menya kiazi kimoja kikubwa na kikate/kisage (grate). Weka siagi (butter) vijiko vidogo vitatu kwenye kikaango (frying pan) na weka kwenye moto hadi iyeyuke. Weka vipande vya viazi kwenye kikaango. Pika kwa joto la wastani kwa dakika 3 – 4. Punguza moto na endelea kupika kwa dakika zingine 4 hadi viazi viwe laini.
  1. Alkalizing Potato Water
Kunywa maji ya viazi gasi moja au mbili kila siku. Ukitumia maji hayo kwa miezi miwili au mitatu mfululizo tatizo la njaa iliyopitiliza (excessive hunger) litatoweka.
Namna ya Kuandaa: Kata viazi viwili vikiwa na maganda yake katika vipande (Slices) na weka kwenye chombo cha kupikia. Weka maji hadi kuvifunika viazi. Chemsha vizi kisha viipue ila usiviondoe kwenye maji mpaka baada ya dakika 15. Mimina maji ya viazi kwenye chombo kingine. Viazi unaweza kuvitupa au kuvila maana nutrients tayari zimeondolewa kwenye hivyo viazi na ziko kwenye maji ya viazi.
Dondoo:
 Ulaji wa kipande cha kiazi kibichi kabla ya kula chakula kinacholetea tatizo la gesi au asidi tumboni (hyperacidity) kutasaidia kukuepusha na tatizo la uyeyushaji chakula tumboni (indigestation).

 Kula kipande cha kiazi kibichi baada ya kuwa umepatwa na tatizo la gesi (acid reflux) kutasaidia kuondoa tatizo hilo katika mfumo wa mwili wako unahusika na usagaji na uyeyushaji wa chakula.

Ulaji wa kipande cha kiazi baada ya kunywa chai au kahawa husaidia kukata asidi kinywani.

 Aina ya milo ya viazi ambaye nimeieleza hapo awali inasaidia sio tu kukabiliana na tatizo la asidi inayopelekea mataizo ya uzito ulizidi au utapiamlo (obesity) bali pia kukabiliana na matatizo yatokanayo na mfumo wa chakula (digestive disorders) kama vile vidonda vya tumbo (ulcers), colitis, diverticultis na Crohn’s disease.

Mimea, matunda na juisi kwa ajili ya tiba ya tatizo la uzito wa mwili
          Pamoja na maelezo niliyokwisha kueleza kuhusu suala hili la uzito au unene kupindukia napenda pia nikueleweshe baadhi ya mimea, matunda na juisi kwa tatizo hilo kama ifuatavyo:
  1. Parachichi (Avocado). Husaidia kupunguza rehamu (cholesterol) mwilini na kuzuia uharibufu wa ini (liver damage preventative). Kula tunda moja au mawili kila siku.
  2. Ndizi (banana). Hupunguza tatizo la kuongezeka uzito, kukosa choo na vidonda vya tumbo. Kula ndizi mbivu kila siku.
  3. Iliki (Ginger root). Hutibu tatizo la kukosa hamu ya kula na tatizo la kutofanya kazi ipasavyo kwa mfumo wa uyeyushaji chakula mwilini. Itumie kama chai na pia weka kwenye chakula unachokula kama kiungo (spice).
  4. Zabibu (Grapes). Hupunguza unene na kuimarisha afya ya mwili. Tengeneza juisi ya zabibu na itumie kutwa nzima huku ukiwa umefunga kula chakula na pia unapaswa kunywa maji glasi 4-5 wakati ukiwa kwenye mfungo huo. Fanya hivyo siku moja kwa wiki na siku 6 zingine kula mlo kamili (balanced meals).
Juisi ya zabibu pia husaidia kutibu magonjwa ya moyo (Heart diseases), kiharusi (strokes) na shambulizi la moyo (heart attacks) na kuziba kwa mishipa ya damu (Arteries anti-clotting). Kwa tiba ya magonjwa hayo kunywa glasi moja ya juisi hiyo iliyotengenezwa kwa zabibu nyekundu (red grapes). Ili kuongeza kasi ya matibabu ya matatizo hayo kula saladi iliyonyunyizwa mafuta ya mizeituni (olive oils) na kunywa juisi ya zabibu nyekundu.
  1. Kiwi (kiwifruit). Hutibu tatizo la kukosa choo (constipation and bowel movements). Ulaji wa matunda 2-4 yakiwa na maganda yake hupelekea kupata choo katika kipindi cha ndani ya masaa 24.
  2. Linseed: hutibu tatizo la kukosa choo. Saga mbegu za linseed kufanya unga. Asubuhi kabla ya kula chakula chochote kunywa maji glasi moja yaliyowekwa unga wa linseed kijiko kimoja cha chakula. Vivyo hivyo kunywa glasi mija ya maji yenye linseed saa moja baada ya kula chakula (main meal).
  3. Mapesheni (passionfruit). Hutibu tatizo la kukosa choo, kutuliza akili (calming effect) na kuzuia maambukizi ya njia ya mkojo (Urinary tract infections –UTI). Kula matunda 2-3 pamoja na mbegu/nyama zake za ndani kila siku.
Unywaji wa juisi iliyotengenezwa kwa mchanganyiko wa mapesheni 2, chungwa moja na vipande viwili vya tikiti maji, asubuhi kabla ya kula chochote ni kinywaji safi kwa kuimarisha afya ya mwili wako.

  1. Prunes. Hutibu tatizo la kukosa choo na hupunguza rehamu mwilini. Kula fresh prunes asubuhi kabla hujala chochote na masaa mawili baada ya kula chakula cha usiku. Ukikosa fresh prunes nunua prunes zilizokaushwa (hupatikana supermarkets) na ziloweke kwenye maji hadi zilainike na zile.
  2. Tikiti (watermelon). Husaidia kupata choo na pia huzuia uharibufu wa ini (liver damage preventative). Kunywa glasi moja ya juisi asubuhi nusu saa kabla hujala chakula chochote.
  3. Juisi ya kupunguza uzito iitwayo ‘Thai Tango’. Weka kwa pamoja kwenye blender: papai lililomenywa gramu 100, pears mawili yaliyomenywa na kukatwa vipande, juisi ya ndimu moja, maji ya mchele (rice milk) 200ml na unga kidogo wa iliki. Blend pamoja kutengeneza juisi.

No comments:

Post a Comment