Tuesday 28 July 2015

Namna Unavyoweza Kutibu Tatizo la Kutopata Choo



 image of constipation  - Woman with constipation or diarrhoea sitting on toilet with her blue pajamas down around her legs - JPG
Tatizo hili husababishwa na kutokula matunda na mboga za majani zakutosha au kutokula vyakula ambavyo havijakobolewa au kuondolewa uasili wake ambavyo kimsingi vina nyuzi (fiber) zinazosaidia kusafisha utumbo mpana (Colon) na kwenda choo ipasavyo. Pia kutokufanya mazoezi ya mwili na kunywa maji ya kutosha (angalau glasi 8 kila siku).


Usipopata choo (angalau mara mbili au tatu kwa siku) au hata kama ni mara moja lakini choo kingi, utakabiliwa na magonjwa mbalimbali. Asilimia takriban 70 ya magonjwa yote hutokana na tatizo la kutokusafishwa vya kutosha kwa utumbo mpana (Colon). Usipopata choo wakati unakula kila siku basi fahamu kwamba ndani ya colon kumegandamana uchafu na sumu za kutosha. Pia nakushauri mara tu ukisikia haja wahi haraka ukaitoe chooni. Kubana choo kwa muda mrefu pia ina madhara kiafya.



Sasa kwa tatizo hilo ni vema kuanza na program ya kusafisha utumbo mpana (Colon) iitwayo ‘Salt Water Flush Program’. Hii uifanye siku ukiwa huna kazi na uko nyumbani. Chukua maji ya vuguvugu lita moja, weka weka chumvi ya baharini (sea salt) ambayo inauzwa madukani au supermarkets. Sio chumvi ya kuchimbwa ardhini bali iliyovunwa kutokana na maji ya bahari. Kunywa hayo maji ndani ya kipindi cha dakika 45 tu.


Kisha lalia ubavu wa kushoto ili kuruhusu maji yatoke tumboni kuingia kwenye utumbo mwembamba. Mara tu ukijisikia kwenda choo nenda mara moja. Endelea kwenda choo mpaka hali ya kusikia choo itakapokoma. Itakuchukua takribani masaa manne hivi.


Baada ya zoezi hilo utafanya hatua ya pili ya Kusafisha utumbo kwa Juisi. Tengeneza juisi yenye mchanganyiko wa matunda matatu, manne au zaidi kati ya matunda haya: Apples, Oranges, Avocados, Raspberries, Papai, Strawberries, Blackberries, Pears, Figs na Prunes. Kunywa kila siku mpaka hali ya kutopata choo itakapoacha. Baada ya hapo sasa uwe na mikakati mizuri ya ulaji chakula (balanced diet).


Juice ingine ukipenda kwa ajili ya tatizo hilo: Blend vipande vya nanasi (kikombe 1), nusu chungwa na papai moja na mbegu zake (ila tu ulimenye). Blend kwenye blender na kunywa.

2 comments: